Pages

Saturday, February 2, 2013

MAAJABU YA DAR... BINTI WA MIAKA 13 AFANYIWA KITCHEN PARTY

Haya ni maajabu kwani familia ya Bwana Masoud Kassim ambao wanaishi Karakata Ukonga Dar wamejikuta wakiingia mikononi mwa polisi mara baada ya kumfanyia KITCHEN PARTY binti yao Rafia Masoud mwenye umri wa miaka 13 ikiwa ni tayari kwa maandalizi ya ndoa ijayo.

Familia hiyo imejikuta ikiingia matatani mara baada ya polisi kupata taarifa kuwa kuna kichen party ya mtoto inafanyika maeneo ya Ukonga Dar.

Binti wa miaka 13 (Rafia Masoud) ambae alifanyiwa kitchen party upande za kushoto akiwa chini ya ulinzi wa polisi
Kwa mujibu wa watu walioweza kushuhudia hiyo kitchen party ya mtoto wa miaka 13 wamesema kuwa kitchen party hiyo ilifanyika tarehe 23/01/2013 lakini kama mambo yangeenda vizuri bila kuingiliwa na polisi ndoa hiyo ilibidi ifungwe leo tarehe 02/02/2013 na hivyo imeshindikana kwa kuwa binti na wazazi wake waliweza kukamatwa wakiwa mikononi mwa polisi.

No comments:

Post a Comment